Thursday, March 21, 2013

17 WASIMAMISHWA KAZI TAZARA

Wafanyakazi 17 wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara), wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi baada ya kuhusishwa na tuhuma za kusafirisha mizigo kwa njia ya magendo kupitia treni ya uokoaji.
Mizigo hiyo ni mbao na mkaa iliyokuwa imehifadhiwa kwenye mabehewa sita ya treni hiyo, ikitokea eneo la Mzenga, wilayani Kisarawe, Pwani usiku wa kuamkia Jumapili.
Gharama za kusafirishia mizigo hiyo ilikuwa ni Sh12 milioni. Kaimu Mkurugenzi wa Tazara, Dk Damas Ndumbaro alisema hatua hiyo ni kupisha uchunguzi.

“Na kuanzia leo (jana), tutakapothibitisha wamehusika wote tunawafukuza kazi, huo ndiyo uamuzi tuliofikia kwa sababu hatuwezi kuendelea kukaa na watu wanaokwenda kinyume na mipango yetu,” alisema Dk Ndumaro.

Pia, Dk Ndumaro alisema hivi sasa mamlaka hiyo imeandaa mpango wa kufanya mabadiliko kuanzia utawala, kuongeza mtaji na kuweka utaratibu wa uwajibikaji kwa viongozi.

“Ili kuifanya Tazara nyingine kuna makubaliano ya mkataba kwa wafanyakazi, kiongozi anasaini kutimiza majukumu kadhaa ndani ya kipindi fulani kama sehemu ya makubaliano, akishindwa lazima awajibike mwenyewe,” alisema Dk Ndumbaro.

Dk Ndumaro alisema iwapo mamlaka itafanikiwa, uzalishaji utapanda kutoka tani 60,000 za mizigo hadi 80,000 kwa mwezi, hatua itakayoongeza kasi mzunguko wa fedha.
“Kiwango tunachoingiza kwa sasa ni dola 4 milioni za Marekani, lakini tutakapofanikiwa bajeti hiyo tutaweza kufikia dola 6 milioni ukilinganisha na matumizi yetu siyo chini ya dola 3 milioni,” alisema

Taarifa zinaonyesha utendaji umeporomoka kwa kiwango kikubwa, kwani tangu bajeti ya mwaka 1986/87 mamlaka ilikuwa inasafirisha tani za mizigo 1.2 milioni na abiria wasiopungua milioni moja, lakini mwaka wa fedha wa 2011/12 mamlaka hiyo imeshuka kwa kiwango cha tani za mizigo 340,000 na abiria wasiozidi 900,000.

STORI KWENYE KURASA ZA MAGAZETI YA LEO MARCH 21 NDIO HIZI HAPA.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
DSC03036 DSC03037
.
.
.
.
.
.
.
.
.
..
..
.

MDAU HII UNAIZUNGUMZIAJE......?

KISA CHA RWAKATALE KUACHIWA NA KUKAMATWA TENA NDIO HIKI HAPA..!

Mkuu wa Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatare na mwenzake Joseph Ludovick Rwezaura wamefutiwa mashtaka ya ugaidi yaliyokuwa yanawakabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kuachiwa huru, lakini walipotoka nje ya chumba cha mahakama “wakakamatwa tena”.

Habari kutoka mahakamani Kisutu zinasema kuachiwa kisha kukamatwa tena kwa watuhumiwa hao kunatokana na makosa ya kisheria yaliyofanywa wakati waliposomewa mashtaka kwa mara ya kwanza.

Makosa hayo ni pale washtakiwa walipoulizwa iwapo wanakubali au wanakana makosa yao, hali mahakama ya Kisutu ikiwa haina uwezo wa kusikiliza kesi za ugaidi.

Washtakiwa hao waliachiwa huru jana saa 3.00 asubuhi na Hakimu Mkazi, Emilius Mchauru baada ya Wakili wa Serikali, Prudence Rweyongeza kuwasilisha hati kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), akiiomba mahakama kuwaachia chini ya kifungu cha 91 (1).

Kifungu hicho kinampa mamlaka Mkurugenzi huyo wa Mashtaka kufuta mashtaka pale anapoona hana sababu ya kuendeleza mashtaka ya mtuhumiwa bila hata ya kutoa sababu zilizosababisha kufanya hivyo.

Hakimu Mchauru alikubaliana na hati hiyo na kuwafutia mashtaka washtakiwa hao waliokuwa wanakabiliwa na kesi namba 37 ya mwaka 2013, iliyokuwa na mashtaka manne yanayohusu vitendo vya ugaidi.

Hata hivyo, baada ya mshtakiwa huyo kuachiwa huru na Hakimu Mchauru, alipotoka nje ya chumba cha mahakama, askari ambao walikuwa wamevaa sare na nguo za kiraia walimkamata Lwakatare ambaye aligoma kukamatwa akidai hadi awepo wakili wake.

Baadaye alifika wakili wake, Peter Kibatala hivyo alikubali kuwekwa chini ya ulinzi. Hivyo askari walimchukua na alipofika karibu na mahakama ya wazi, alifungwa pingu na baadaye kwenda kuhifadhiwa ndani ya gari la polisi akiwa chini ya ulinzi mkali.

Ilipofika saa 4:10 asubuhi, Lwakatare na mwenzake, Ludovick walipandishwa tena kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi, Aloyce Katemana na kusomewa kesi mpya PI namba 96 yenye mashtaka manne yanayofanana na yale ya awali ya ugaidi.

Akisoma hati hiyo mpya ya mashtaka, Wakili Rweyongeza alidai kuwa washtakiwa hao walifanya kosa hilo la jinai kinyume na kifungu cha 384 cha sheria ya kanuni ya adhabu, sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho 2002.

Rweyongeza alidai kuwa Desemba 28, mwaka jana katika eneo la King’ong’o, Wilaya ya Kinondoni, washtakiwa hao kwa pamoja walikula njama ya kumdhuru kwa sumu Dennis Msacky ambaye ni Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi, kinyume na kifungu cha 227 cha sheria ya kanuni ya adhabu.

Wakili huyo wa Serikali katika shtaka la pili alidai kuwa washtakiwa hao kwa pamoja walikula njama ya kufanya kosa la jinai kinyume na kifungu cha sheria cha 24 (2) cha sheria dhidi ya ugaidi sura ya 21 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Alidai kuwa washtakiwa hao, Desemba 28,2012 walishirikiana kupanga njama za kumteka nyara Msacky kinyume na kifungu cha 21 cha sheria inayopinga ugaidi.

Katika shtaka la tatu, wanadaiwa kufanya mkutano wa vitendo vya kigaidi kinyume na kifungu cha 5 (a) cha sheria namba 21 inayopinga ugaidi iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Aliendelea kudai kuwa siku ya tukio, washtakiwa hao walipanga na kushiriki katika mkutano wa kupanga kitendo cha ugaidi cha utekaji nyara dhidi ya Msacky.

Kwa mujibu wa shtaka la nne, Lwakatare anadaiwa kuhamasisha vitendo vya ugaidi.
Aliongeza kudai kuwa siku hiyo ya tukio, Lwakatare akiwa mwenye nyumba, akijua, aliruhusu mkutano kati yake na Ludovick ufanyike katika nyumba yake kwa lengo la kuhamasisha vitendo vya kigaidi dhidi ya Msacky.

Kabla ya kufutwa kwa kesi hiyo, Hakimu Mchauru alitakiwa kutoa uamuzi kama washtakiwa hao watapata dhamana ama la, kutokana na hoja zilizokuwa zimewasilishwa na mawakili wa pande zote mbili.

Hata hivyo, suala hilo halikujadiliwa baada ya Hakimu Katemana kusema kwamba hakuwa na muda wa kulisikiliza kwani alikuwa anawahi kesi nyingine.Kesi hiyo sasa imeahirishwa hadi April 3, mwaka huu na mawakili wa pande zote mbili watapata fursa ya kujadili suala hilo.

Lwakatare anatetewa na mawakili watano, Peter Kibatala, Mabere Marando, Abdallah Safari, Nyaronyo Kicheere na Tundu Lissu.
Chanzo mwananchi.

Zilizosomwa zaidi