Saturday, March 16, 2013

HAYA NDIO YANAENDELEA MAHAKAMNI NCHINI KENYA

Ni maandamano ya amni yanayofanywa na wafuasi wa Laira Odinga
baada ya kuwasilisha malalamiko yake mahakamani.

ZISOME STORI KUBWA KATIKA KURASA ZA MBELE NA ZA NYUMA KWENYE MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI 16 MARCH.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

UPENDO KILAHIRO AFUNGUKA KUHUSU BIASHARA YA NYIMBO MTANDAONI.

Mwimbaji wa nyimbo za Injili nchini, Upendo Kilahiro amewataka wamiliki wa kampuni za kuuza kazi za wasanii mitandaoni, kuhakikisha wanatoa elimu ya kutosha kwa wasanii ili kuweka uwazi katika biashara hiyo.
Upendo alisema kwamba wasanii wengi hawana uelewa katika matumizi ya mtandao, hivyo bado kuwa gizani kuhusu umiliki wa kazi zao zilizopo katika mtandao na namna zitakavyowalipa.
"Sisi tunaimba muziki wa Injili, baadhi yetu tunajua matumizi ya mtandao na wapo wasiojua, tunawasaidia vipi hawa? Pia muziki wa kizazi kipya na taarabu ni hivyo hivyo, nadhani elimu inahitajika zaidi ili msanii aweze kujua haki yake kikamilifu,"
"Licha ya kuwepo hilo, bado hakuna uwazi ni namna kazi zetu zitauzwa, nadhani wapo wengi wanaojiuliza hili. Uwazi unahitajika zaidi ili kuwa na amani kati ya sisi na wamiliki wa mtandao husika."

ODINGA KUTUA MAHAKAMANI LEO.

Muungano wa CORD unaoongozwa na Raila Odinga umesema kuwa leo utawasilisha malalamiko yake katika Mahakama ya Juu kupinga ushindi wa Uhuru Kenyatta aliyetangazwa mshindi katika uchaguzi wa machi 4.
Mwanasheria wa Cord,  James Orengo alisema  kwamba  Muungano huo umepokea sehemu kubwa ya nyaraka na maelezo uliyohitaji kutoka  Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).
Alisema nyaraka hizo ndizo ambazo zinawawezesha kuwasilisha malalamiko  ya kupinga kuchaguliwa kwa Uhuru Kenyatta kuwa Rais.
Alisema miongoni mwa yaliyokabidhiwa CORD ni karatasi zilizotumiwa kuhesabu kura, Fomu 34, 35 na 36 na pia sajili ya wapigakura.
Jaji Isaac Lenaola anayesikiliza kesi hiyo aliagiza wahusika warudi Jumatatu kuthibitisha ikiwa wote wametii matakwa na kwa maagizo zaidi. CORD ilikuwa imeshtaki IEBC na Safaricom lakini Safaricom ikaondolewa baada ya kuitikia matakwa yote ya muungano huo.
Kesi hiyo ilikuwa imewasilishwa na Eliud Owallo ambaye ni mkuu wa kampeni wa muungano huo.
Hivyo Rais Mteule Uhuru Kenyatta hataweza kuapishwa hadi Mahakama Kuu isikilize na kuamua kesi zote zinazopinga kuchaguliwa kwake.
Kamati inayoshughulikia kuapishwa kwa Rais mteule imeweka mpangilio kabambe wa sherehe hiyo, ikitilia maanani aina tofauti za uamuzi utakaotolewa na mahakama katika kesi ambayo muungano wa Cord uliwasilisha  katika Mahakama ya Juu.
Kamati hiyo, inayosimamiwa na Mkuu wa Utumishi wa Umma, Francis Kimemia imeweka mpangilio wa kuapishwa kwa Rais kwa kuzingatia uamuzi wa kesi hiyo.
Kimemia alisema mpangilio huo mpya utatolewa na unahakikisha hakuna pengo litakalotokea katika ubadilishanaji wa mamlaka.
Kamati hiyo imeweka Aprili 16 kuwa tarehe ya kuapishwa kwa Rais mteule, endapo kesi ya Cord itatupiliwa mbali na Mahakama ya Juu.

Zilizosomwa zaidi