| Zambia | 1 - 1 | Ethiopia | |
| Nigeria | 1 - 1 | Burkina Faso | |
Monday, January 21, 2013
MPAKA SASA DIWANI ALIYEFUMANIWA HUKO IRINGA, AGOMA KWENDA HOSPITALI KUTIBIWA
Kama
ni kituko cha mwaka basi hiki pia ni kituko cha aina yake pamoja na
diwani wa kata ya Ifunda jimbo la Kalenga wilaya ya Iringa mkoani
Iringa Mheshimiwa Elia Mgwila kufumaniwa na kukatwa sikio moja na
kung'olewa meno ila bado diwani huyo ambae ni majeruhi ameendelea
kugoma katukatu kwenda Hospital kutibiwa majeraha hayo.
Mbali
ya kuwagomea ndugu na marafiki hao bado diwani huyo amegoma kwenda
kituo cha polisi kufungua shitaka hilo na kudai kuwa yote anamwachia
mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi na vyote vilivyopo duniani .
Wakati
diwani huyo akigoma kufika Hospital kutibiwa taarifa zinadai kuwa
jeshi la polisi ambalo lilikuwa likimshikilia bwana mwenye mke
aliyefumaniwa na diwani huyo mkazi wa kijiji cha Ifunda kibaoni pamoja
na mdogo wake na mkewe wameachiwa huru na jeshi la polisi ambalo
lilikuwa likiwashikilia kwa tukio hilo la kumjeruhi diwani .
Huku
habari za kipolisi zikidai kuwa watuhumiwa hao wameachiwa huru
kutokana na diwani huyo kugoma kufungua kesi juu ya shambulio hilo
la mwili.
| Diwani Elia Mgwila aliyesimama |
| Mpiga kura akigonga mlango wa diwani bila mafanikio |
Nyumba ya aliyofumaniwa diwani huyo na mke wa mtu hii hapa
| Hapa ni nyumbani kwa mheshimiwa mlango ukiwa umefungwa huku ufunguo ukiwa nje |
Mwananchi akitoka kumwona diwani huyo bila mafanikio leo
GARI LA SERIKALI LANASWA LIKIWA NA PEMBE ZA NDOVU ARUSHA
GARI aina ya Toyota VX linaloelezwa kuwa mali ya Serikali limekamatwa na polisi likiwa limebeba pembe za ndovu.
Gari hilo lilikamatwa juzi saa 3:00 usiku katika Kijiji cha
Kigongoni katika Mji wa Mto wa Mbu, wilayani Manyara baada ya gari hilo
kupinduka.
Vyanzo vya uhakika kutoka ndani ya Jeshi na Polisi
zimeeleza kuwa askari wa jeshi hilo aliyekuwa akiendesha gari hilo
anashikiliwa na polisi.
Uchunguzi umebainisha kuwa ndani ya gari hilo kulikuwa na meno ya tembo na watu wengine watatu ambao walikimbilia porini na baadhi ya nyara hizo.
Uchunguzi umebainisha kuwa ndani ya gari hilo kulikuwa na meno ya tembo na watu wengine watatu ambao walikimbilia porini na baadhi ya nyara hizo.
Habari hizo zimedai bado kuna utata kuhusu gari
lililokuwa likitumiwa na maofisa hao kwa kuwa kibao cha namba za gari
hilo kinasomeka kwa namba za kiraia lakini vioo vimechorwa namba za
Serikali, huku Mkurugenzi Mkuu wa Tanapa akisema pia kulikuwa na namba
za JWTZ.
Kulingana na taarifa kutoka ndani ya Jeshi la
Polisi, kukamatwa kwa gari hilo kulitokana na Askari wa Shirika la
Hifadhi za Taifa Tanzania (Tanapa), Hifadhi ya Ziwa Manyara kudokezwa na
raia wema.
Inaelezwa kuwa baada ya askari hao kudokezwa,
walianza kufuatilia nyendo za maofisa hao ndani ya hifadhi na
walipogundua wanafuatiliwa, gari hilo liliongeza mwendo kuelekea Mji wa
Mto wa Mbu.
Hata hivyo, kutokana na mwendokasi wa gari hilo na kutokuwa wazoefu kulinganisha na Askari wa Tanapa, gari la maofisa hao lilipinduka lilipofika Kijiji cha Kigongoni nje kidogo ya Mto wa Mbu.
Hata hivyo, kutokana na mwendokasi wa gari hilo na kutokuwa wazoefu kulinganisha na Askari wa Tanapa, gari la maofisa hao lilipinduka lilipofika Kijiji cha Kigongoni nje kidogo ya Mto wa Mbu.
“Baada ya kupekuliwa lilikutwa na pembe mbili za
ndovu na uchunguzi wa awali umethibitisha maofisa waliokimbia
walifanikiwa kutoroka na pembe nyingine tatu,” kilidokeza chanzo hicho.
Kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kulitokana na wananchi kumtilia shaka yeye na wenzake gari lao lilipopata ajali kwa kitendo cha watu wawili waliokuwepo kwenye gari hilo kuonekana wakihamisha mizigo na kukimbilia porini.
Kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kulitokana na wananchi kumtilia shaka yeye na wenzake gari lao lilipopata ajali kwa kitendo cha watu wawili waliokuwepo kwenye gari hilo kuonekana wakihamisha mizigo na kukimbilia porini.
“Matairi mawili ya gari yalipasuka lakini ajabu ni
kwamba wananchi walipojitokeza kusaidia majeruhi, wawili kati yao
walinyanyua mizigo isiyojulikana na kukimbilia porini huku wakimwacha
mwenzao aliyevaa sare za jeshi akisubiri garini,” alisema mtoa taarifa
wetu.
Kwa mujibu wa mashuhuda, wakati wa ajali hiyo,
mtuhumiwa alikuwa amevaa jaketi la JWTZ pamoja na suruali ya jinsi akiwa
na bunduki aina ya Rifle.
Katika msako uliofanywa na polisi kwa kushirikiana na wananchi, pembe mbili zaidi za ndovu zilikutwa zikiwa zimefichwa karibu na eneo la ajali.
Katika msako uliofanywa na polisi kwa kushirikiana na wananchi, pembe mbili zaidi za ndovu zilikutwa zikiwa zimefichwa karibu na eneo la ajali.
Mkurugenzi mkuu wa Tanapa, Allan Kijazi
alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lakini akasema hana taarifa kamili
kwani yuko Tanga na wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na
Mazingira.
“Ni kweli nimearifiwa juujuu tu, nasubiri taarifa
kamili lakini nimeambiwa tu hilo gari lilipinduka wakati wakifukuzana na
askari wetu, lakini mnaweza mkapata taarifa zaidi polisi,” alisema
Kijazi.
Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe alisema hajapata taarifa hiyo, hivyo asingeweza kutolea maoni kwa namna yeyote.
Chanzo: Mwananchi
Chanzo: Mwananchi
AIBU KUBWA STENDI KUU YA MABASI UBUNGO BAADA YA UKUTA KUBOMOKA
SEHEMU ya ukuta wa kituo cha mabasi ya kwenda mikoani cha Ubungo, jijini
Dar es Salaam, leo alfajiri umeanguka na kuyaharibu vibaya magari
zaidi ya ishirini yaliyokuwa yameegeshwa nje ya eneo hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alisema kuwa idadi ya magari yaliyopatwa na ajali hiyo yanakadiriwa kufikia 24 ambapo watu watatu wanasemekana wamejeruhiwa.

Baadhi ya magari yaliyoangukiwa na ukuta.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alisema kuwa idadi ya magari yaliyopatwa na ajali hiyo yanakadiriwa kufikia 24 ambapo watu watatu wanasemekana wamejeruhiwa.

Baadhi ya magari yaliyoangukiwa na ukuta.
Magari mbalimbali yakiwa chini ya kifusi.
Gari aina ya Noah likiwa limegandamizwa na zege.
Hii ndiyo hali halisi ya tukio lilivyokuwa.
Gari aina ya Toyota likiwa limebonyezwa na zege.
Watu wakiangalia magari yao.
Kenyela akiongea jambo juu ya ajali hiyo.
likuwa ni hasara tupu.
Hali ilikuwa ni mbaya katika zahama hiyo ya alfajiri ya leo.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
Israel Magesa Wakili Magesa aliyeko (pichani) amefariki dunia ghafla leo asubuhi. Wakili Magesa, ambaye ni mmiliki wa kampuni y...
-
GARI aina ya Toyota VX linaloelezwa kuwa mali ya Serikali limekamatwa na polisi likiwa limebeba pembe za ndovu. ...
-
-
Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bo...
-
Nimepokea mwaliko wa kikao maalumu cha kikao cha fedha na uongozi wa tarehe 3/01/2014 kikao kufanyika tarehe 06/01/2013 saa nane mchana ...






