Wednesday, December 12, 2012
STORI YA NGASSA KUHAMIA SUDANI IKO HAPA......KWA HABARI ZAIDI INGIA HAPA
Mbali na kuiaibisha nchi, klabu hizo kwa pamoja
zinaona kitendo hicho kuwa ni utovu wa nidhamu na usumbufu kwa viongozi
wa timu hiyo ya Sudan waliokuja nchini kukamilisha zoezi hilo.
Simba na Azam zilitangaza kukubaliana kumuuza
Ngassa kwa ada ya Dola 100,000 (Sh157 milioni). Katika makubaliano ya
mkataba wa mchezaji huyo, El Merreikh ilidaiwa kuwa tayari kumpa Ngassa
mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya Dola 75,000 (Sh118 milioni).
Jana alipaswa kufanyiwa vipimo vya afya jijini Dar
es Salaam chini ya viongozi wa timu hiyo ya Sudan, lakini katika hali
ya kushangaza hakutokea.
Akikaririwa na vyombo mbalimbali vya habari juzi,
Ngassa alisema hayuko tayari kujiunga na El Merreikh kwa vile siyo Simba
wala Azam iliyomshirikisha katika zoezi hilo.
Hata hivyo kauli ya Ngassa inapingana na aliyoitoa
wakati akiwa na kikosi cha Timu ya Taifa Bara (Kilimanjaro Stars),
akiitaka Simba iache kumbania kuchezea timu hiyo ya Sudan.
Makamu Mwenyekiti wa Simba Godfrey Nyange alisema wamesikitishwa na kitendo alichofanya Ngassa na kwamba watamwita ili kumhoji.“Hatufahamu nini kimempata mpaka sasa. Kwanza hao viongozi wa El Merreikh yeye binafsi ndiye aliyeongea nao na kufikia makubaliano,” alisema Nyange.
Makamu Mwenyekiti wa Simba Godfrey Nyange alisema wamesikitishwa na kitendo alichofanya Ngassa na kwamba watamwita ili kumhoji.“Hatufahamu nini kimempata mpaka sasa. Kwanza hao viongozi wa El Merreikh yeye binafsi ndiye aliyeongea nao na kufikia makubaliano,” alisema Nyange.
Nyange alisema wameshangazwa na uamuzi wa Ngassa
wa kubadilika ghafla. “Pengine kuna kitu hapa, amebadilika ghafla,”
aliongeza Nyange aliyeteuliwa kuzungumzia suala hilo pia kwa niaba ya
Azam.
Alisema kitendo hicho kimeiaibisha Simba na Taifa
kwa jumla kwani ni sawa na kuwafungia milango wachezaji wengine wenye
nia ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi.
Wakati huohuo, Juma Nyoso ameendelea kuisisitizia klabu yake ya Simba kusitisha mkataba wake haraka ili ajiunge na timu ya Coastal Union ya Tanga.
Wakati huohuo, Juma Nyoso ameendelea kuisisitizia klabu yake ya Simba kusitisha mkataba wake haraka ili ajiunge na timu ya Coastal Union ya Tanga.
Uongozi wa Simba ulimpeleka Nyoso kujifua na
kikosi cha timu ya vijana kwa madai ya kushuka kiwango na utovu wa
nidhamu.Hata hivyo beki huyo anayecheza nafasi ya kati, aligoma
kutekeleza agizo hilo la kwenda kujiunga na kikosi B.
CHANZO; MWANANCHI GAZETI
CHANZO; MWANANCHI GAZETI
WAFANYAKAZI NGORONGORO KUFUKUZWA KAZI
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Hamis Kagasheki ametangaza
kuwachukulia hatua za kinidhamu maofisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro (NCAA) waliokwamisha mradi wa kuwasaidia wafugaji wa hifadhi
hiyo ulioahidiwa na Rais Jakaya Kikwete mwaka 2008.Akizungumza na wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro na viongozi wa NCAA mara baada ya kuelezwa kuhusu kukwama kwa mradi huo, Balozi Kagasheki alisema lazima hatua kali zichukuliwe dhidi ya viongozi hao.
“Haiwezekani mradi ulioahidiwa mwaka 2008 leo hii ukwame, waliohusika kuukwamisha ni lazima wakae pembeni. Ninakwenda Dar es Salaam ila wakae wakijua kuwa barua zao zinakuja” alisema Kagasheki na kuongeza;
“Kabla sijaondolewa wizarani kutokana na matatizo kama haya, mtaondoka ninyi kwanza.…, kukwama kwa mradi huu kutawafanya wananchi wamchukie Rais Kikwete na wanasiasa,” alisema Balozi Kagasheki.
HIKI NDIO KICHANGA KILICHOTUPWA JIJINI DAR
Kichanga hicho cha jinsi ya kike, kinakadiriwa kuwa na umri wa
siku mbili, kimekutwa katika machimbo ya mchanga maeneo ya
Majohe, Gongo la Mboto.
Polisi wanaendelea na juhudi za kumtafuta muhusika
MKURUGENZI MTENDAJI BUNDA AZOMEWA.
KAIMU Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Bunda, Dinah Rweyemamu
juzi alipatwa na wakati mgumu pale alipozomewa na wananchi
wakimshinikiza ashuke jukwaani kufuatia wananchi hao kutoridhika na
majibu aliyokuwa akiyatoa kwa maswali yao.
Dinah alifikwa na zahama hiyo muda mfupi baada ya
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Abdallah Bulembo kumwita jukwaani
ajibu maswali hayo yaliyoelekezwa kwake wakati wa mkutano wa hadhara wa
chama hicho uliofanyikia katika eneo la kituo cha zamani cha mabasi
mjini Bunda.
Swali lililomletea kizaazaa kaimu mkurugenzi huyo
ni lile lililotolewa na Alfred Ndowa aliyetaka kujua sababu za kukithiri
kwa michango kwa shule za msingi na sekondari hasa wakati wa
kuandikisha wanafuzni wa darasa la kwanza.
Bulembo alimwita Dinah jukwaani ambapo katika
kujibu alisema dhamana ya kutokuwapo au kuwapo kwa michango mashuleni
imo mikononi mwa kamati zao za shule.Kufuatia kauli hiyo ,wananchi
walianza kumzomea kaimu mkurugenzi huyo wakisema hajui kitu na kumtaka
Bulembo amshushe.
WAMISRI KUPIGIA KURA KATIBA

Maandamano hasimu kuhusu kura ya maoni juu ya katiba mpya
Wananchi wa Misri wanaoishi
katika nchi za kigeni, wameanza
kupigia kura ya maoni rasimu juu ya katiba
ambayo imezua hali
ya mvutano nchini humo
Subscribe to:
Posts (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
Israel Magesa Wakili Magesa aliyeko (pichani) amefariki dunia ghafla leo asubuhi. Wakili Magesa, ambaye ni mmiliki wa kampuni y...
-
GARI aina ya Toyota VX linaloelezwa kuwa mali ya Serikali limekamatwa na polisi likiwa limebeba pembe za ndovu. ...
-
-
Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bo...
-
Nimepokea mwaliko wa kikao maalumu cha kikao cha fedha na uongozi wa tarehe 3/01/2014 kikao kufanyika tarehe 06/01/2013 saa nane mchana ...






























