
Monday, November 19, 2012
BOB JUNIOR AKANA KUWA SHOGA
Baada ya fununu nyingi kusambaa mtaani kuwa staa wa Bongo Fleva, Raheem Nanji ‘Bob Junior’ kuwa ni Shoga sasa ameogea waziwazi.Akizungumza kupitia kipindi cha runinga moja usiku wa Ijumaa iliyopita, Bob Junior alisema chanzo cha yeye kudaiwa ni shoga ni wimbo wake maarufu wa Oyoyo.
Alisema mara baada ya kuitoa video ya wimbo wake huo akiwa anakata sana mauno, watu walikuwa wakimpigia simu, wengine wakimtumia meseji kwamba, anaonekana ni ‘chakra’ maana anayaweza sana mauno.
“Watu wanasema mimi ni shoga, lakini si kweli. Kisa kilianzia kwenye ule wimbo wangu wa Oyoyo. Unajua katika video ya ule wimbo nilikata sana mauno, watu wakaamini mimi shoga."
“Wengine walikuwa wakinitumia hata meseji wakiamini hivyo. Kwa hiyo sababu kubwa ni ile video tu, watu wana mambo ya ajabu sana,” alisema Bob Junior huku watu alioongozana nao usiku huo wakitingisha vichwa kukubaliana naye.
Ishu ya Bob Junior kuonekana ni chakra pia iliwahi kusababisha amfikishe kortini kwenye Mahakama ya Mwanzo Kinondoni, Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu akidaiwa kumtukana msanii huyo matusi ya nguoni likiwemo hilo la ushoga.
Katika kesi hiyo iliyofikishwa kwenye mahakama hiyo kwa mara ya kwanza Mei 4, 2011 na kusikilizwa na Hakimu Mfawidhi Mariam Masamalo, Wema alihukumiwa kulipa faini ya shilingi 40,000 au kwenda jela miezi 6 ambapo alifanikiwa kulipa.
AMANI CONGO BADO MATATANI
Serikali ya Jamuhuri ya
Kidemokrasia ya Congo, imetupilia mbali matakwa yaliyotolewa na
wapiganaji wa waasi wa kuanzisha mazungumzo ya amani, na kukariri kuwa
itaendelea kuulinda mji wa Goma, Mashariki mwa nchi hiyo.
Waasi wa M23 wamesemekana kuukaribia mji huo huku maelfu ya raia wakikimbia makwao.Mapema hii leo, wapiganaji hao walitoa ilaani ya saa ishirini na manne kwa serikali ya nchi hiyo kuanzisha mazungumzo, ya amani la sivyo wataendelea na vita hivyo.
Baraza la usalama la umoja wa mataifa limelaaini hatua hiyo ya waasi wa M23 ya kuendelea na mapigano huku wakielekea mji wa Goma.
Mapigano hayo yametajwa kuwa mabaya zaidi tangu mwezi Julai Mwaka huu katika eneo hilo lenye utajiri mkubwa wa madini.
Barabara za mji wa Goma hazikuwa na raia kama kawaida na magari ya kijeshi na yale ya umoja wa mataifa ndiyo yaliyokuwa yakizunguka mji huo.
SEKRETARIETI CCM YAJA KIVINGINE
SEKRETARIETI mpya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imeapa kusimamia
utekelezaji wa Ilani ya chama hicho tawala kwa kufuatilia mienendo ya
watendaji wakuu wa Serikali wakiwamo mawaziri.Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa mpango huo wenye lengo la kuongeza ufanisi wa Serikali, utawabana pia wakuu wa mikoa, wilaya na watendaji wengine wanaosimamia utekelezaji wa Ilani hiyo.
Alisema ikibainika mtendaji yeyote wa Serikali anabaronga katika uwajibikaji wake, sekretarieti hiyo itamjulisha Rais Jakaya Kikwete na kumshauri awafukuze kazi.
“Lengo ni kuhakikisha kila mmoja anawajibika kwa nafasi yake na endapo itabainika watendaji wanaboronga, sekretarieti haitasita kumfahamisha Rais ili awatimue ama kuwaondoa katika majukumu yao,” alisema.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
Israel Magesa Wakili Magesa aliyeko (pichani) amefariki dunia ghafla leo asubuhi. Wakili Magesa, ambaye ni mmiliki wa kampuni y...
-
GARI aina ya Toyota VX linaloelezwa kuwa mali ya Serikali limekamatwa na polisi likiwa limebeba pembe za ndovu. ...
-
-
Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bo...
-
Nimepokea mwaliko wa kikao maalumu cha kikao cha fedha na uongozi wa tarehe 3/01/2014 kikao kufanyika tarehe 06/01/2013 saa nane mchana ...
