Monday, November 5, 2012
HIZI NDIO KAULI 18 ALIZOZISEMA OBAMA KABLA YA UCHAGUZI LEO HII.
RADIO CALL, FUNGUO ZA GARI ALIYOKUWA NAYO KAMANDA BARO IMEPATIKANA.
Mbali na
simu hiyo, jeshi hilo pia limefanikiwa kupata ufunguo wa gari la marehemu
Barlow ambaye aliuawa wakati akimsindikiza mwanamke mmoja aliyeitwa Doroth
Moses walipokuwa wakitoka kwenye kikao cha harusi ya ndugu yake.
Kaimu
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Lili Matola, alisema jana kwamba vitu hivyo
vilipatikana vikiwa vimefichwa katika shimo la majitaka katika nyumba moja
iliyopo maeneo ya Nyashanya.
Pia jeshi
hilo limefanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa wengine wawili wanaodaiwa kuhusika
katika mauaji hayo na Kamanda Matola alisema wataunganishwa kizimbani na
wengine watano Novemba 15, mwaka huu.
Alisema
watuhumiwa hao wawili (majina tunayahifadhi kwa sasa), mmoja wao akiwa ni ndugu wa mtuhumiwa namba
moja katika mauaji hayo, ndio waliotaja sehemu vilikokuwa vimefichwa vitu hivyo
baada ya kuhojiwa.
“Baada ya
kuonyesha vilipokuwa vimefichwa, ilibidi kumtaarifu mwenye nyumba ambaye alitoa
idhini ya kubomolewa kwa shimo hilo la majitaka na mmoja wa watuhumiwa aliingia
na kutoa ‘radio call’ pamoja na funguo za gari la marehemu,” alisema Kamanda
Matola.
Alisema kuwa
baada ya kutekeleza mauaji hayo, mtuhumiwa namba moja alitoa maelekezo ya wapi
pa kuficha vifaa hivyo. Kabla ya kuficha simu hiyo, waliitenganisha na betri
yake.
Kamanda
Matola alisema katika msako waliofanya nyumbani kwa watuhumiwa hao, pia
walikuta sare za moja ya kampuni ya ulinzi
pamoja na magwanda ya mgambo.
Alisema kuwa
vitu vingine vilivyokamatwa ni kofia mbili, moja ikiwa ya polisi na nyingine ya
kampuni ya ulinzi pamoja na vifaa mbalimbali vinavyotumika kwa ajili ya kufanyia
uhalifu.
Alisema
mmoja wa watuhumiwa aliwahi kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 jela,
alichokitumikia kuanzia mwaka 2006 baada ya kukutwa na makosa ya unyang’anyi
kwa kutumia silaha. Hata hivyo, alisema aliachiwa huru mwaka 2010 baada ya
kukata rufani Mahakama Kuu na kuachiwa huru.
Alisema
katika mahojiano na polisi, mtuhumiwa huyo alisema alishawishiwa na kaka yake
kufanya kazi hiyo ya ujambazi.
Mbali na
watu hao, Matola alisema polisi pia inamshikilia mtu mmoja (jina tunalihifadhi)
mkazi wa Nyakabungo akituhumiwa kufadhili kundi hilo la majambazi.
MICHAKATO YA MAISHA
(Mr. Ponciano Vanpyeree.)
Ukiachana na mambo ya Shule, haya ni mambo ambayo kijana huyu anjihusisha nayo.
Yeye anadai hii mambo iko damuni hivyo baada ya shule anafanya hivyo unavyoona hapo juu
RIPOT KUTOKA UN
Ripoti kutoka umoja wa mataifa inaonesha kuwa takribani
asilimia 70 ya watu wanaoishi maisha ya chini ya dola moja
kwa siku ni wanawake.
asilimia 70 ya watu wanaoishi maisha ya chini ya dola moja
kwa siku ni wanawake.
DIWANI, KATIBU WA CHADEMA MWANZA KUTIWA RUMANDE.
Mahakama yawatia ndani Diwani, Katibu wa CHADEMA
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimepata pigo kubwa
baada ya Mahakama kuwaweka ndani Diwani wa Kata ya Kirumba jijini
Mwanza, Dan Kahungu pamoja na Katibu wa Chadema Wilaya ya Ilemela, John
Anajus kwa kosa la kukaidi amri halali ya mahakama, iliyozuia uchaguzi
wa nafasi ya Meya na Naibu wake katika Manispaa hiyo.
Mbali na viongozi hao wa Chadema kupelekwa mahabusu ya Gereza Kuu la Butimba, pia Mahakama hiyo ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, imeagiza wakamatwe kisha kufikishwa mahakamani Mkurugenzi wa Oganaizesheni wa Chadema taifa, Benson Kigaila na aliyekuwa Meya wa Jiji la Mwanza ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Tendaji ya chama hicho, Josephat Manyerere kwa kosa hilo hilo la kudharau amri ya mahakama.
Amri hiyo imetolewa hii leo na Hakimu Mkazi Mfawidhi mkoani Mwanza, Angelo Rumisha, kufuatia kesi namba 69/2012 iliyopo mahakamani hapo dhidi ya watuhumiwa sita kutoka chama hicho, ambapo alisema mara baada ya watuhumiwa hao kukamatwa mahakama itatoa hukumu yake kwa pamoja.
Akitoa amri hiyo, Rumisha alisema mahakama haiwezi kutoa adhabu kwa baadhi ya watuhumiwa, na kwamba agizo la kutaka wakamatwe Manyerere na wenzake ni kutaka mahakama iheshimiwe, mara inapotoa amri zake halali kwa mujibu wa sheria za nchi.
Kupitia kesi hiyo yenye namba 69/2012, Rumisha aliwataja wengine wanaotakiwa kukamatwa na jeshi la polisi kisha kufikishwa mahakamani hapo ni pamoja na Mkurugenzi huyo wa Oganaizesheni ya Chadema taifa, Kigaila, Katibu wa mwenezi wa Chama hicho wilaya ya Ilemela, Kalod Majura pamoja na mkuu wa Mdhamini wa Chadema.
Awali ilidaiwa mahakamani hapo na wakili wa upande wa mlalamikaji mahakamani hapo, Salum Magongo kwamba watuhumiwa wote kwa pamoja walishiriki kikao cha kutangaza uamzi wa kumfukuza udiwani, Henry Matata wa Chadema (kata ya Kitangiri), kabla pingamizi lililokuwa limewasilishwa mahakamani na diwani huyo halijatolewa maamuzi na mahakama.
“Mteja wangu Henry Matata aliweka pingamizi mahakamani baada ya Kamati Tendaji ya Chadema kutangaza kumvua uanachama kinyume cha taratibu. Lakini watuhumiwa wote wa kesi hii walishiriki kuvunja sheria kwa kumtangaza kumfukuza udiwani”, alidai mahakamani hapo wakili Magongo.
Aidha, Wakili huyo aliendelea kudai kuwa, kwa kufanya hivyo washtakiwa hao walipuuza amri halali ya mahakama iliyotolewa na mahakama Septemba 15 mwaka huu, kinyume cha sheria na taratibu.
Hata hivyo, hakimu Rumisha aliamuru diwani huyo wa kata ya Kirumba, Kahungu pamoja na Anajus waende mahabusu katika gereza la Butimba, hadi hapo watuhumiwa wengine watakapokamatwa na jeshi la polisi kisha kuhukumiwa kwa pamoja.
Wadadisi wa mambo wanadai kwamba, kosa la kupatikana kudharau amri halali ya mahakama adhabu yake ni kwenda miezi sita, au kulipa faini, hivyo viongozi hao wa Chadema huenda wakahukumiwa kutumikia adhabu kadri itakavyoamriwa na mahakama
Mbali na viongozi hao wa Chadema kupelekwa mahabusu ya Gereza Kuu la Butimba, pia Mahakama hiyo ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, imeagiza wakamatwe kisha kufikishwa mahakamani Mkurugenzi wa Oganaizesheni wa Chadema taifa, Benson Kigaila na aliyekuwa Meya wa Jiji la Mwanza ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Tendaji ya chama hicho, Josephat Manyerere kwa kosa hilo hilo la kudharau amri ya mahakama.
Amri hiyo imetolewa hii leo na Hakimu Mkazi Mfawidhi mkoani Mwanza, Angelo Rumisha, kufuatia kesi namba 69/2012 iliyopo mahakamani hapo dhidi ya watuhumiwa sita kutoka chama hicho, ambapo alisema mara baada ya watuhumiwa hao kukamatwa mahakama itatoa hukumu yake kwa pamoja.
Akitoa amri hiyo, Rumisha alisema mahakama haiwezi kutoa adhabu kwa baadhi ya watuhumiwa, na kwamba agizo la kutaka wakamatwe Manyerere na wenzake ni kutaka mahakama iheshimiwe, mara inapotoa amri zake halali kwa mujibu wa sheria za nchi.
Kupitia kesi hiyo yenye namba 69/2012, Rumisha aliwataja wengine wanaotakiwa kukamatwa na jeshi la polisi kisha kufikishwa mahakamani hapo ni pamoja na Mkurugenzi huyo wa Oganaizesheni ya Chadema taifa, Kigaila, Katibu wa mwenezi wa Chama hicho wilaya ya Ilemela, Kalod Majura pamoja na mkuu wa Mdhamini wa Chadema.
Awali ilidaiwa mahakamani hapo na wakili wa upande wa mlalamikaji mahakamani hapo, Salum Magongo kwamba watuhumiwa wote kwa pamoja walishiriki kikao cha kutangaza uamzi wa kumfukuza udiwani, Henry Matata wa Chadema (kata ya Kitangiri), kabla pingamizi lililokuwa limewasilishwa mahakamani na diwani huyo halijatolewa maamuzi na mahakama.
“Mteja wangu Henry Matata aliweka pingamizi mahakamani baada ya Kamati Tendaji ya Chadema kutangaza kumvua uanachama kinyume cha taratibu. Lakini watuhumiwa wote wa kesi hii walishiriki kuvunja sheria kwa kumtangaza kumfukuza udiwani”, alidai mahakamani hapo wakili Magongo.
Aidha, Wakili huyo aliendelea kudai kuwa, kwa kufanya hivyo washtakiwa hao walipuuza amri halali ya mahakama iliyotolewa na mahakama Septemba 15 mwaka huu, kinyume cha sheria na taratibu.
Hata hivyo, hakimu Rumisha aliamuru diwani huyo wa kata ya Kirumba, Kahungu pamoja na Anajus waende mahabusu katika gereza la Butimba, hadi hapo watuhumiwa wengine watakapokamatwa na jeshi la polisi kisha kuhukumiwa kwa pamoja.
Wadadisi wa mambo wanadai kwamba, kosa la kupatikana kudharau amri halali ya mahakama adhabu yake ni kwenda miezi sita, au kulipa faini, hivyo viongozi hao wa Chadema huenda wakahukumiwa kutumikia adhabu kadri itakavyoamriwa na mahakama
Subscribe to:
Posts (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
Israel Magesa Wakili Magesa aliyeko (pichani) amefariki dunia ghafla leo asubuhi. Wakili Magesa, ambaye ni mmiliki wa kampuni y...
-
GARI aina ya Toyota VX linaloelezwa kuwa mali ya Serikali limekamatwa na polisi likiwa limebeba pembe za ndovu. ...
-
-
Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bo...
-
Nimepokea mwaliko wa kikao maalumu cha kikao cha fedha na uongozi wa tarehe 3/01/2014 kikao kufanyika tarehe 06/01/2013 saa nane mchana ...
