.Huyo ni panya anayepatikana mkoani Morogoro katika chuo kikuu cha Sokoine ambapo hutumika katika kutambua mtu aliyeathirika na TB. Panya huyo hutambua kwa kunusa makohozi ya mtu.
Kwa sasa panya hao wanhudumia hospitali 13 nchini.
Michuano ya kikapu kombe la taifa imeanza leo huko
jijini Tanga katika kiwanja cha CCM Mkwakwani
ambapo timu ya Tanga imekipiga na timu kutoka Pwani
na mchezo wa pili umekuwa kati ya Arusha na Lindi.
Katibu msaidizi wa shirikisho ls kikapu Tanzania TBF
Michael Malue amesema maandalizi yako vizuri sana
na mambo ni mazuri,
Amesema timu kutoka mikoa 13 zimeshawasili jijini Tanga.
Mapacha wa kundi la P-Square la nchini Nigeria hatimaye wamefunguka
kuzikanusha tetesi kuwa walimtoa kafara mama yao mzazi ili watajirike na
kufanikiwa zaidi kimuziki.
Katika mahojiano exclusive na gazeti la Vanguard la nchini Nigeria, Peter na Paul wamesema,
“Basi, ni mbaya sana kusikia kuwa watu wanatushutumu kwa kuhusika na
kifo cha mama yetu. Hatumlamu mtu yeyote. Watu wako huru kusema chochote
wanachotaka kusema. Tunashangaa kama kuna kitu chochote
kitakachotufanya tuchukue maisha ya mama yetu mpendwa.
Maisha yake hayawezi kupimwa kwa fedha na umaarufu. Hivyo jibu letu
kwa swali hili ni kwamba hatuhusiki na kifo cha mama yetu. Tunakilaumu
tu kifo kilichomchukua mbali nasi ambacho kama si chenyewe watu
wasingekuwa wanatunyooshea vidole. Alifariki baada ya ugonjwa wa muda
mfupi.”
HATIMAYE usafiri wa treni ndani yaT Jiji la Dar es Salaam kuanza
rasmi leo na kupokewa kwa furaha na wananchi waliojitokeza kuutumia. Waziri mwakyembe ameonekana ndani ya gogo akifurahia kuzinduliwa kwa usafiri huo
WAZIRI wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe yuko mkoani Mbeya kwa ziara ya
siku mbili ikiwa ni mwendelezo wa kutembelea mikoa na vitongoji
vilivyopo katika fukwe za Ziwa Nyasa.