Wednesday, September 26, 2012
Okwi kuikosa mechi ya Simba na Yanga. Shirikisho la soka nchini TFF, limethibitisha adhabu ya Emmanuel Okwi ya kuikosa mechi ya Simba na Yanga itakayochezwa Oct 3. Hii ni baada ya Okwi kupewa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya JKT Ruvu. Afisa habari wa shirikisho hilo Bw Boniface Wambura amesema "Okwi atakosa jumla ya mechi tatu ikiwemo ya oct 3, pia atalipa faini ya laki tano"
Vijana wajitokeza uchaguzi CCM. Wakati chama cha mapinduzi kikiendelea na uchaguzi wa chama, vijana wenye umri wa miaka arobaini (40) na wasomi wa elimu ya juu ndio waliojitokeza kuchukua fomu. Akiongea katibu mwenezi wa chama hicho Nape Nnauye, amesema kuwa chama hicho kimepanga kuleta mabadiliko katika utendaji, "Nimeshuhudia kuona asilimia 50 ya waliochukua fomu ni vijana" .
Baada ya wizara ya usafirishaji kupiga marufuku uchimbaji dawa barabarani, sasa vyo vilivyojengwa katika vituo mbalimbali vyatia aibu kwa uchafu. Miongoni mwa vyoo vinavyoongoza kwa uchafu ni vile vilivyojengwa katika mzani wa msata huko pwani. Hii imeelezwa na baadhi ya wasafiri waliopita katika kituo hicho.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
Israel Magesa Wakili Magesa aliyeko (pichani) amefariki dunia ghafla leo asubuhi. Wakili Magesa, ambaye ni mmiliki wa kampuni y...
-
GARI aina ya Toyota VX linaloelezwa kuwa mali ya Serikali limekamatwa na polisi likiwa limebeba pembe za ndovu. ...
-
-
Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bo...
-
Nimepokea mwaliko wa kikao maalumu cha kikao cha fedha na uongozi wa tarehe 3/01/2014 kikao kufanyika tarehe 06/01/2013 saa nane mchana ...