Thursday, September 20, 2012

Raisi Kikwete azindua rasmi ujenzi wa daraja la Kigamboni jijini Dar.

Mwanafunzi ajifungua wakati akifanya mtihani wa Hisabati. Huko mkoani kagera hapo jana, mwanafunzi amejifungua mtoto wa kiume alipokuwa akifanya mtihani wa Hisabati ambao ndio ulikuwa wa mwisho katika safari ya elimu ya shule ya msingi. Wazazi na walimu wamesema walikuwa hawajui kama mwanafunzi huyo alikuwa ana ujauzito.

DAWA ZA ARV's SI KITU TENA. Wizara ya afya ikishirikiana na watafiti wamebaini kuwa zile dawa za kupunguza makali ya VVU hazina nguvu thabiti dhidi ya vvu bali kuleta usugu kwa wagonjwa. Hivyo imezitaka hospitali zote nchini kuondoa dawa hizo katika ghara zao za dawa.

Rais Jakaya Kikwete amezindua rasmi mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni leo hii jijini Dar. Lengo ni kurahisisha usafiri kwa wakazi waishio Kigamboni.

Milioni 73 zapatikana kwa mechi moja. Katika michuano ya ligi kuu Tanzania inayoendelea, hapo jana katika mchezo kati ya Simba na Ruvu JKT katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam, jumla ya mil 73 zimekusanywa katika mchezo huo.

Shule ya sekondari Maranda iliyopo nchini Kenya imefungwa Kwa mda baada ya mabweni mawili kuungua. Tatizo lilosababisha kuungua kwa mabweni hayo bado halijafahamika, wakati huohuo shule ya sekondari ya wasichana iliyopo jirani na Maranda sec. imefungwa kwa tahadhari ya kutokea kwa ajari nyingine kama hiyo.

Serikali yaingilia ujenzi wa benki za wananchi. Akiongea waziri mkuu Mh. Mizengo pindi, amesema kuwa serikali inaangalia uwezeka wa kuziwezesha halmashauri zenye ari ya kuanzishwa kwa benki za wananchi.

Bidhaa kutoka nje ya nchi kuzorotesha soko la ndani. Haya yamesemwa na wawekezaji nchini kuwa bidhaa zinazoingia nchini kutoka nje ni nyingi sana. Hivyo wameiomba serikali kudhibiti uingizaji wa bidhaa kutoka nje ili kukuza soko la ndani na kujiongezea pato la taifa.

Mashindano ya Redd's miss Temeke kufanyik kesho jijini Dar. Siku ya kesho katika ukumbi wa PTA katika uwanja wa maonesho ya mwalimu Nyerere. Mashindano hayo yataambatana na burudani ya muziki kutoka kwa bendi ya Mashujaa ya jijini Dar.

Simba na Yanga kupata neema ya mabasi ya kisasa. Kampuni ya bia Kilimanjaro imepanga kuzikabidhi timu za Simba na Yanga mabasi ya kisasa leo hii.

Wanafunzi wapatao 4,000 wamekosa mkopo kwa mwaka wa masomo 2012/2013 kutokana na ufinyu wa bajeti. Akiongea kaimu Mkurugenzh wa bodi hiyo Bw. Asangye Bangu amesema jumla ya wanafunzi 49,895 walituma maombi kwa bodi ya mikopo, kati yao wanafunzi 33,050 ndio walikidhi vigezo lakini waliopata mkopo ni wanafunzi 29,113. Asilmia 31.9 ni wasichana wakati asilimia 68.0 ni wavulana.

Zilizosomwa zaidi