Monday, September 17, 2012

Makamu wa pili wa Zanzibar Dk Seif Idd amesema Zanzibar ndio inayofaidi muungano. Amesema Zanzibar inanufaika na muungano huo kwani ndio unaotumika katika shughuli za maendeleo katika eneo hilo.

Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza yatisha kwa ongezeko la watu. Hayo yamebainika hapo jana wakati waziri mkuu Mizengo Pinda alipofanya ziara wilayani humo. Pinda amesema idadi ya watu wilayani humo ni kubwa ukilinganisha na ukubwa wa ardhi iliyopo.

Madaktari waliogoma waiomba radhi serikali. Hii ni kutokana na mgomo walioufanya na kusababisha athari kubwa kwa wagonjwa, waliojutia mgomo huo ni madaktari waliokuwa chini ya madaktari bingwa ambao walifukuzwa kazi. Wamekiri kwa kusema mgomo ni kitu kisichofaa katika jamii.

Waziri mkuku akosa kurushiwa mawe alipokuwa akifanya mkutano na wakazi wa mwanza. Ni katika ziara aliyoifanya mkoani mwanza. Story kamili endelea kufuatilia.

Timu ya watoto wa jangwani Young Afrika wanaendelea na mazoezi yao kuiva mtibwa katika michuano ya ligi kuu Tanzania. Wakati wa mazoezi yao leo hii, kocha wa timu hiyo amesema Kicha walichokipokea Yanga kutoka kwa Prisons ya huko Mbeya jumamosi iliyopita, ilikuwa ni maandalizi mabaya ya timu hiyo. Yanga imeahidi kuonesha tofauti katika michezo ijayo.

Wakazi wa kijiji cha Kwadelo kilichopo wilayani Kondoa mkoani Dodomg walalamika kwa kukosa huduma ya maji. Richa ya kuwa Mkoa huo una asili ya ukame, serikali imewaacha solemba wakazi wa kijiji hicho kwani hata visima havijachimbwa kijijini hapo. Akiongea mkazi wa kijiji hicho ambaye jina lake halikutajwa amesema, inawalazimu wanawake kutembea umbali mrefu usikt wa manane kutafuta maji jambo ambalo ni hatari kwa maisha yao. Serikali ikishirikiana na wakazi wa Kwadelo imeombwa kulishughulikia tatizo hili mapema kwani wamekuwa wakipata shida hiyo kwa mda mrefu.

Wazazi katika maeneo mbalimbali nchini wameendelea kukemea vitendo vya udanganyifu ambao huwa unajitokeza kwa wanafunzi katika kipindi cha mitihani. Waalimu na wasimamizi watakiwa kuwa makini sana katika kusimamia ili kuepusha swala la wanafunzi kuingia kidato cha kwanza wakati hawajui kusoma na kuandika.

Waziri wa ujenzi na miundombinu Dk John Magufuri, amesema bilion 500 zimetumika katika ujenzi na ukarabati wa miundombinu jijini Dar. Amesema mgawanyo wa billion 500 umepelekwa katika ujenzi wa barabara ya Msata kuelekea Bagamoyo, pamoja ujenzi wa daraja la huko kigamboni.

Wakati tukiendelea na wiki ya nenda kwa usalama barabarani, wananchi watakiwa kuwa makini pindi watumiapo barabara ili kupunguza ajari na vifo vitokanavyo na ajari za barabarani. Kwa mkoa wa Dar es salaam ajari za pikipiki zimeripotiwa kuwa nyingi katika kipindi cha August. Wakati huohuo waendesha pikipiki wilayani kasulu mkoani Kigoma wanaendelea kunufaika na wiki hii ya nenda kwa usalama kwani chuo cha mafunzo ya ufundi FDC wilayani humo, kimeanda kozi fupi ya wiki moja ya kujifunza namna kuendesha pikipiki na kupewa cheti maalum kitakachowasaidia wahitimu hao kupata Leseni ya udereva kwa urahisi.

Zilizosomwa zaidi