Tuesday, September 11, 2012

Kata ya kipawa yakabidhiwa mdawati 500 na visima vya maji. Aliyekuwa waziri mkuu nchini, Edward Lowasa amekabidhi madawati 500 na visima viwili vya maji shule ya msingi Kinyuri iliyopo kata ya Kipawa jijini Dar es salaam. Hatua hii ni katika mpango wa kuboresha mazingira ya kupata elimu nchini.

Wachimbaji wadogowadogo wa madini kuruhusiwa Geita. Baada ya machimbo ya dhahabu yaliyopo katika kijiji cha Mgusu mkoani Geita kufungwa mwaka 2009 kutokana na ajali iliyotokea, sasa machimbo hayo yamefunguliwa na kuwaruhusu wachimbaji wadogowadogo kuanza kuchimba madini katika eneo hilo

Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF Dk Ibrahim Lipumba amesema, ili kuimalisha uchumi serikali haina budi kuweka utaratibu na mfumo mzuri wa kukusanya kodi. Imefahamika kuwa sekta nyingi nchini hazilipi kodi kikamilifu na hivyo kuisababishia serikali hasara kubwa.

Simba sports club kuitwaa Ngao ya jamii katika uwanja wa taifa jijini Dar baada ya kuichala Azam FC ya Dar magoli 3-2. Azam ilifanikiwa kupata magoli yote mawili katika kipindi cha kwanza wakati simba walikuwa nyuma kwa goli moja hadi kipindi cha mapumziko. Lakini katika kipindi cha club ya Simba ilijihakishia ushindi baada ya kuongeza magoli mawili na kuyafanya matokeo kuwa Simba 3-2 Azam

Mbio za mwenge wa uhuru zinazoendelea nchi nzima leo zimefika huko wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Mwenge huo utalala wilayani kasulu katika uwanja wa Umoja uliopo Kasulu mjini.

Katika mashambulizi yanayoendelea huko Tana River nchini Kenya, Imeripotiwa kuwa vijiji vinne vimeshambuliwa tena asubuhi leo hii.

Watu 14 watajwa kwa tuhuma za kubomoa kontena bandarini katika yadi ya Kampuni ya Oryx na kuiba Madini vipande 19, Mafuta ya Petrol lita 360 na Disel lita 60. Jeshi la polisi mkoa wa Dar es salaam limethibitisha kuwajamata watu hao.

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Bernad Membe, amethibitishiwa mpaka sahihi kati ya Tanzania na Malawi katika ziwa Nyasa. Akiongea na wazee waishio mwambao mwa ziwa Nyasa wamesema kuwa mpaka upo katikati ya Ziwa Nyasa na wala sio katika upande wa Tanzania.

Simba na Azam kukipiga leo katika uwanja wa taifa jijini Dar katika michuano ya Ngao ya jamii

Zilizosomwa zaidi