Monday, September 10, 2012
Kumbukumbu za kihistoria leo tar 11 septemba. 1853-Simu ya kutumia umeme ilitumika kwa mara ya kwanza. 1875-Gazeti la kwanza la cartoon liliandikwa. 1885-Moses Hopkins alitajwa kuwa Waziri wa Liberia. 1888-Mwanasiasa mkongwe nchini Algentina Domingo Sarmiento aliuawa. 1895-Kombe la ligi kuu FA, liliibiwa huko Birmingham.
Baada ya vuta nikuvute kati ya jeshi la polisi na waandishi wahabari jijini Dar, sasa waandishi wa habari waruhusiwa kufanya maandamano hapo kesho. Kamanda wa polisi Suleiman Kova amethibitisha kuwepo kwa maandamano. Maandamano hayo ni ya kupinga mauaji ya mwandishi Daud Mwangosi yaliyotokea wiki iliyopita huko iringa. Kilele cha maandamano hayo itakuwa katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar.
Chama cha wananchi CUF kimeanzisha mikutano ya hadhara ya mfulurizo. Katika mkutano uliofanywa na cha hicho jana katika viwanja vya jangwani jijini Dar, Dk Ibrahim Lipumba ameishauri serikali kuweka sera itakayowasaidia wakulima wadogowadogo ili kuimarisha uchumi wa nchi na sio vinginevyo. Aliongeza kuwa nchi nyingi duniani kama vile Denmark zimeweza kujiimalisha kiuchumi kwa kuanza kuimarisha uzalishaji wa wakulima wadogowadogo. Kama serikali na wanaharakati wote watashindwa kufanyia kazi mawazo haya, bado nchi itaendelea kuwa na hali ngumu kiuchumi.
Richa ya kuwa mashindano ya riadha yamekamilika na kufungwa hapo jana katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam, changamoto mbalimbali zimeweza kujitokeza katika kipindi chote cha mashindano. Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa vifaa ambapo iliwalazimu washiri kukimbi bila kuvaa viatu na wanawake kuvaa sketi badala ya bukta za kiriadha. Hii ni kwa jinsi gani serikali na wizara ya michezo kushindwa kuandaa mashindano haya kikamilifu. Ni vizuri kwa mashindano yajayo kuandaliwa vizuri ili kuukuza mchezo huv wa riadha.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Zilizosomwa zaidi
-
Israel Magesa Wakili Magesa aliyeko (pichani) amefariki dunia ghafla leo asubuhi. Wakili Magesa, ambaye ni mmiliki wa kampuni y...
-
GARI aina ya Toyota VX linaloelezwa kuwa mali ya Serikali limekamatwa na polisi likiwa limebeba pembe za ndovu. ...
-
-
Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bo...
-
Nimepokea mwaliko wa kikao maalumu cha kikao cha fedha na uongozi wa tarehe 3/01/2014 kikao kufanyika tarehe 06/01/2013 saa nane mchana ...

