Friday, September 7, 2012

Tarehe ya leo katika kumbukumbu Kihistoria. 1796-kulikuwa na vita ya Mapinduzi nchini Ufaransa. 1962-Algeria kupata uhuru.

WAZO LANGU. Haya makundi mbalimbali vya muziki maarufu kama "Mduara" yanatoa wapi maadili na ujasiri wa watoto wa kike kukata viono hadharani wakiwa wamevalia Khanga moja? Kama ni uhuru basi wasanii Tanzania wamepewa uhuru uliopitiliza hadi kufikia hatua ya wasanii wenyewe kushindwa kujiheshimu. Hivi kizazi cha leo watoto wanajifunza nini kupitia mchezo kama huo? Ni vizuri basi wasanii walioachiwa huru kuhusika katika muziki huo kufuata maadili, kwani kushindwa kwao kufuata maadili kinachofuata ni kujiabisha wenyewe na taifa kwa ujumla. Pia serikali iliangalie suala hili kwa jicho la pili ili kulinusuru taifa katika wimbi hili zito la "Khanga moja ndembendembe".

Wizara ya usafiri na uchukuzi imesema usafiri wa treni kwa wakazi wa jijini Dar es salaam utaanza Octoba mwaka huu. Imesemwa kuwa hata kama muundombinu huo utakuwa haujakamilika, usafiri huo lazima uanze. Shughuli za ukarabati wa rili kutoka Stesheni hadi Ubungo unaendelea vizuri.

Waziri mstaaf Fredrick Sumaye, amewataka polisi kuacha kutumia silaha na nguvu za ziada katika kupambana na raia bali kutumia busara. Suala hili limetokana na tabia ya polisi kuwapiga raia kwa kutumia silaha zao bila hata kujali. Chanzo:Mwananchi

Kundi la boko haram limelipua minara ya simu za mkononi nchini Nigeria.

Mgomo wa walimu nchini Kenya unaendelea sasa ikiwa ni siku ya nne. Wakati mgomo huu unaendele wanafunzi wa darasa la nane waliokuwa wanatarajia kuanza mitihani, wamehakikishiwa na wizara ya elimu nchini humo kuwa mitiahani itaanza jumatatu ijayo

Zaidi ya waumini 300 wa dini ya Kiislam wameandamana jijini Dar es salaam. Maandamano ya waumini hao ni kuitaka serikali kuwaachia huru waislamu wote waliokamatwa kwa madai ya kupinga shughuli ya Sensa. Kutokana na kuandamana kwao, tayari serikali imetoa tamko la kuwaachia huru wote waliokuwa wakishikiliwa na jeshi la polisi.

Katika hatua za kupunguza ajari nchini, serikali imekuja na vidhibiti mwendo vya kisasa. Baada ya serikali kuleta vidhibiti mwendo (speed governer) katika gari za kubeba Abiria kwa mara ya kwanza na kushindwa kufanikiwa kupunguza ajari, sasa yaamua kuleta vidhibiti mwendo vipya.

Waziri wa ujenzi Dk John Magufuli amesema atawachukulia hatua wahandisi wote watakaobainika kukiuka maadili ya taaluma zao. Hii ni baada ya kubaini kuwa wahandisi wengi hawatumii taaluma zao kikamilifu katika utendaji wa kazi. Chanzo:Mwanachi

Miili ya wanajeshi wa kulinda amani wa Jeshi la wananchi JWTZ waliofariki wiki iliyopita huko Darfur nchini Sudan imewasili leo nchini. Baadhi ya Askari wa jeshi la wananchi wamefika kuipokea miili ya marehemu hao katika uwanja wa ndege wa Air Wing jijini Dar es salaam.

Zilizosomwa zaidi