Wednesday, September 5, 2012

Chama cha Mapinduzi CCM kupitia katibu mwenezi wa chama hicho Bw Nape Nnauye, amikitaka chama cha Chadema kuhusika katika vifo vinavyotokea wakati wa maandamano yanayofanywa na wafuasi wa chama hicho kioapokuwa kinafanya mikutano yake katika maeneo mbalimbali nchini.

Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania imetangaza kuwepo kwa Elinino mwaka huu. Mamlaka hiyo imetangaza uwdepo wa mvua nyingi na za mfululizo katika maeneo mengi nchini kuanzia mwezi wa kumi.

Kama una habari yako, tangazo, shuguli za harusi na unataka Dj na Mc kwa ajili ya kazi yako, wasiliana nami kwa namba 0713914416

Tume ya kukusanya maoni kuhusu katiba mpya ikiongozwa na ndg Warioba imetua wilayani Kasulu mkoani Kigoma, tume hiyo itaanza kukusanya maoni ya wakazi wa wilaya ya kasulu leo Alhamis 6 august katika uwanja wa umoja Kasulu mjini kuanzia sa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni. Wananchi wote wanaombwa kuhudhuria na kushiriki katika shughuli hiyo moja kwa moja au kwa kuandika waraka na kuufikisha kwa tume hiyo.

Serikali nchini Tanzania imeandaa mpango maalum wa kutoa elimu kwa wafanyakazi wa selta ya afya, mpango huo unalenga kupunguza maambukizi ya Virusi vya ukimwi na magonjwa mengine yanayoenea kwa njia ya kutoa damu kwa kutumia sindano.

Wakati leo mgomo wa waalimu wa shule za msingi na sekondari ukiingia siku ya nne nchini Kenya, wahadhiri nao wa vyuo vikuu wamepanga kuanza mgomo leo nao wakiitaka serikali kuwaongezea mishahara. Chanzo:BBC

Mwanza nao waja na wimbo wao unaokwenda kwa jina la Mwanza All Star. Hii ni baada ya wasanii kutoka mkoani Kigoma kupiga wimbo wao Leka dutigite, basi wasanii jijini mwanza akiwemo Sajna, Kulea, King Fenya na wengine kupitia Mbunda records, nao wamekuja na wimbo wao.

Mwanza nao waja na wimbo wao unaokwenda kwa jina la Mwanza All Star. Hii ni baada ya wasanii kutoka mkoani Kigoma kupiga wimbo wao Leka dutigite, basi wasanii jijini mwanza akiwemo Sajna, Kulea, King Fenya na wengine kupitia Mbunda records, nao wamekuja na wimbo wao.

Tume ya kukusanya Maoni ya Katiba mpya inayoongozwa na Wariobo, imefika wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Tume hiyo itaanza kukusanya maoni ya wakazi wa wilaya hii kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na moja za jioni katika uwanja wa umoja ndani ya Kasulu mjini.

Zilizosomwa zaidi