Monday, August 27, 2012

Diamond Plutnum kufanya kolabo na J Martin. Hii ni baada ya kufanya shoo kali katika mashindano ya Big Brother Africa na hivyo kuanza kualikwa sehemu mbalimbali kutoa burudani. Hivi sasa Diamond amesema tayari ameshaingiza voko za wimbo huo kwa producer Marco Chali na sasa amesubiri kuingiza voko za J Martin ambaye hivi sasa yupo nchini Marekani

Nape aigomea Chadema. Baada ya mbunge wa Ubungo, John Mnyika kutoa siku saba kabla ya kwenda mahakamani,kuitaka CCM kuilipa Chadema fidia ya Sh. Bilion 3 kutokana na tuhuma zilizotolewa kuwa Chadema hicho kinapokea mabilioni kutoka nje, Katibu mwenezi wa CCM, Nape Nnauye amewaeleza waandishi wa habari kuwa chama hakotayari kulipa fidia yoyote, "kama ni kwenda mahakamani waende hata kesho wasisubiri siku saba kwani watapoteza mda" pia amemtaka katibu wa Chadema, Wilbrod Slaa kutoa uthibitisho kwa madai aliyoyatoa kuwa CCM inaingiza siraha nchini. Kwa upande wa kulipwa fidia, Nape ameitaka Chadema kuilipa CCM Sh. Bilion 3.1

Kituko kimetokea mkoani Tabora baada ya ziara ya kushtukiza iliyofanywa na mkuu wa mkoa katika stendi ya mabasi ya mkoa huo. Katika usiku wa kuamkia siku ya Sensa mkuu wa mkoa huo Bi Fatuma Mwasa aliitembelea stendi hiyo na kuikuta ina uchafu usioelezeka jambo lililomfanya bi Fatuma kuwakurupusha Watendaji wa wilaya ya Tabora mjini usiku huo kufika na kuanza kufanya usafi mara moja, muda huohuo. Kwa aibu waliyoipata watendaji hao, waliamua kuwapa tenda vijana wakafanya usafi ndani ya stendi usiku huo.

Wekundu wa Msimbazi Simba sports club, inatarajia kumalizia mchakato wa usajili wa mchezaji Koman Bill Keita kutoka nchini Mali kwa thamani ya dola 30 za kimarekani. Beki huyo atachukua nafasi ya Mussa Mude ambaye amekuwa majeruhi kwa mda mrefu.

Timu ya mpira wa miguu Azam, imemtimua rarmi kiungo kutoka Kenya George Odhiambo 'BLACKBERY' kutokana na utovu wa nidhamu katika timu hiyo. Msemaji wa timu hiyo amesema Odhiambo hakufika mazoezini takribani siku nne bila kutoa taarifa. Aliongeza kuwa nafasi yake itachukuliwa na mchezaji mwingine mapema iwezekanavyo.

Waislam mkoani Kigoma katika maeneo ya Mwandiga nje Kidogo ya mji wa Kigoma, wameisusia shughuli ya sensa na kugoma kuhesabiwa kwa kuamua kukaa msikini. Kitendo hiki kimefanywa na baadhi ya Masheh katika msikiti wa Mwandiga kuwahamasisha waislam kwenda kukaa msikitini. Walipotaka kuhojiwa, walikataa, na hawakuongea lolote.

Kocha wa club Arsenal aanza kuliona pengo lililoachawa na kiungo Vern Persie aliyehamia club ya Manchester United. Hii ni baada ya kutoka suluhu katika mechi iliyochezwa jana kati ya Arsenal na Stoke City ambapo mchezo ulimalizika bila timu yoyote kuuona mlango wa mwenzake.

Baada ya Jeshi la Polisi mkoani Morogoro kuingilia maandamano yaliyokuwa yanafanywa na Chadema mkoani humo, mtu mmoja aripotiwa kupoteza maisha.

Mshukiwa mkuu wa Al Shabaab, Aboud Rogo ameuawa nchini Kenya. Aboud alikuwa na kesi ya Ugaidi na kupanga njama za mashambulizi.

Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu yakabiliwa na tuhuma za Ubadhilifu wa pesa. Imeripotiwa kuwa vigogo katika bodi hiyo hujilipa mishahara minono, kigogo mwingine aajiri ndugu zake 11 wasio na sifa. Mpaka sasa pesa iliyokusanywa na Bodi hiyo ni bilion 9 tu, na zaidi ya bilion 300 hazijakusanywa bado. Chanzo: Jamii forum

Shughuli ya sensa inaendelea siku ya pili sasa lakini changamoto nyingi zinawakabiri makarani wa sensa. Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na Uhaba wa vifaa vya kazi, kukosa sale na vitambulisho jambo ambalo inawawia vigumu sana kutambulika wanapofika katika baadhi ya kaya.

Baada ya wafuasi wa Chadema mkoani Morogoro kutaka kufanya maandamano kuelekea kwenye mkutano unaofanyika uwanja wa ndege, imewalazima Polisi mkoani humo kutumia mabomu ya machozi kutuliza maandamano hayo.

Zilizosomwa zaidi