Wednesday, August 15, 2012

Chadema, Nnauye sahani moja. Chadema wampeleka Katibu wa CCM itikadi na uenezi, Nape Nnauye kwa msajiri wa vyama kuhusiana tuhuma alizozisema kwa Chadema kutumia pesa za harambee katika vuguvugu za mabadiriko licha ya kupata fedha kutoka kwa wafadhili wa nje.

Wakati Vikao vya Bunge vikielekea kumalizika leo hii, wananchi wamewataka wabunge kurejea majimboni kwao ili kuweza kuongea na wananchi na kupanga mikakati ya maendeleo kwa pamoja na sio kukimbilia jijini Dar

Kambi ya upinzani Bungeni imeiomba serikali kuwaanika mawaziri ambao wamefisha mabilioni ya pesa nchini Uswis. Waziri kivuli wa fedha kutoka chama cha maendeleo na demokrasia (chadema) bw Zitto Kabwe amesema jana bungeni kuwa sh 315.5 bilion imewekwa katika benki nchini Uswis. Aliongeza kuwa Benk ya Uswis ilipotoa repoti Juni mwaka huu, ilionesha kuwa bil315.5 kufichwa nje na mawaziri na akiwemo kiongo wa ngazi ya juu serikalini.

Mbunge wa Mwanza Bw Andrew Chenge amewaomba wabunge wote kujadili na kuweka wazi ni lugha ipi itumike katika kufundishia shule za msingi. Amesema kuwa lugha ya kiswahili ndio inayotumika kwa sasa lakini viongozi na wabunge wanaoipa lugha hiyo kipaumbele bado wanawapeleka watoto wao katika shule zinazofundisha kiingereza tu. Chenge ameongeza kuwa hali kama hii inasababisha matabaka ya kielimu katika jamii.

Mechi ya kirafiki iliyokuwa inachezwa kati ya Tanzania na Botswana imemalizika kwa kufungana gori tatu kwa tatu. Magori ya Tanzania yamepatikana kupitia wachezaji watatu ambao ni Mrisho Ngasa, Kazimoto pamoja na Nyoni.

Simba yaipiga Azam 2-1. Pia simba imewatambulisha wachezaji wapya.

Mafunzo yanayoendele kuhusu Sensa yaendelea kuleta hali ya sitofahamu katika maeneo mbalimbali ambapo baadhi ya washiriki katika semina wanaondolewa. Mkoani Dar es salaam baadhi ya washiriki katika semina baada ya siku ya tatu bila kulipwa hata shilingi.

Zilizosomwa zaidi